Papa Celestino I
(Elekezwa kutoka Papa Celestine I)
Papa Celestino I alikuwa Papa kuanzia tarehe 10 Septemba 422 hadi kifo chake tarehe 24 Julai 432[1]. Alitokea Campania, Italia na baba yake aliitwa Priscus.
Alimfuata Papa Boniface I akafuatwa na Papa Sixtus III.
Akiwa na juhudi za kulinda na kupanua Kanisa, alianzisha uaskofu katika visiwa vya Britania akaunga mkono Mtaguso wa Efeso katika kumuita Bikira Maria "Mama wa Mungu" dhidi ya mafundisho ya Nestori[2].
Alipambana pia na uzushi wa Upelaji [3] na kupigania nidhamu[4][5] pamoja na kudhibiti farakano la Novatianus[6].
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sikukuu yake ni tarehe 27 Julai[7] lakini pia 6 Aprili au 8 Aprili.
Tazama pia
Maandishi yake
- Opera Omnia katika Patrologia Latina ya Migne pamoja na faharasa
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
- Kuhusu Papa Celestino I katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki
- Saint Celestine I Archived 13 Machi 2012 at the Wayback Machine.
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Celestino I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz