Waashuru
Waashuru (kwa Kiaramu ܣܘܪܝܝܐ) ni kabila la Kisemiti la watu wa Mesopotamia kaskazini, ambao leo kwa kiasi kikubwa wanaishi nje ya nchi yao asili (hasa katika Iraq na Syria za leo, pamoja na maeneo madogo ya Uturuki na Iran), hasa Marekani, Ulaya Magharibi na Australia.[1][2][3][4][5][6]
Kwa jumla duniani kote wanakadiriwa kuwa kati ya milioni 2 na 4.25. Wengi wao ni Wakristo (hasa Kanisa Katoliki la Wakaldayo na Kanisa la Waashuru la Mashariki), na kwa sababu hiyo wamedhulumiwa na watawala mbalimbali kwa karibu miaka 2000 mfululizo.[7]
Waashuru wana historia tukufu upande wa ustaarabu na siasa kwa kuwa walirithi na kueneza utamaduni wa Wasumeri na Waakadi ambao ndio wa kwanza duniani katika mambo mengi.
Hasa dola la Ashuru lilistawi kati ya karne ya 24 KK na karne ya 7 KK liliposhindwa na Wakaldayo wa Babuloni (605 KK).
Biblia inazungumzia mara nyingi habari za dola hilo lililokuwa tishio kwa Waisraeli na mataifa mengi ya Mashariki ya Kati kwa muda mrefu.
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
- Assyrian people, Britannica Online
- A virtual Assyria: Cyberland Archived 16 Novemba 2007 at the Wayback Machine.
- A virtual Assyria: Christians from the Middle East Archived 27 Septemba 2007 at the Wayback Machine.
- Traditional Assyrian Costumes Archived 19 Novemba 2012 at the Wayback Machine.
- Assyrian Iraqi Document Projects
- Who Are Assyrians?
- Assyrian History
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Waashuru kama enzi zake au matokeo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |