Cabo Verde

Cabo Verde (Kiingereza: Cape Verde) ni nchi ya visiwa katika bahari ya Atlantiki mbele ya pwani ya Afrika ya Magharibi.

Jamhuri ya Cabo Verde
República de Cabo Verde (Kireno)
Bendera ya Cabo Verde
Bendera
Nembo ya Cabo Verde
Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Unidade, Trabalho, Progresso (Kireno)
"Umoja, Kazi, Maendeleo"
Wimbo wa taifa: Cântico da Liberdade (Kireno)
"Mkarara wa Uhuru"
Mahali pa Cabo Verde
Mahali pa Cabo Verde
Ramani ya Cabo Verde
Ramani ya Cabo Verde
Mji mkuu
na mkubwa nchini
Praia
20°54′ N 156°22′ W
Lugha rasmiKireno
Kikaboverde
SerikaliJamhuri
 • Rais
 • Waziri Mkuu
José Maria Neves
Ulisses Correia e Silva
Eneo
 • Eneo la jumlakm2 4 033[1]
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023603 901[1]
Pato la taifaKadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 2.598[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 4 503[2]
Pato halisi la taifaKadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 5.717[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 9 909[2]
Maendeleo (2021)Ongezeko 0.662[3] - wastani
SarafuEscudo ya Cabo Verde

Umbali wake na Senegal ni km 460.

Jiografia

Eneo la visiwa vyake kwa jumla ni km² 4,033.

Funguvisiwa lake lina visiwa 15 katika vikundi viwili:

Miji

Mji mkuu ni Praia katika kisiwa cha Santiago.

Miji mikubwa zaidi ni (takwimu za mwaka 2010): Praia (wakazi 127,832), Mindelo (wakazi 70,468), Santa Maria (wakazi 23,839), Assomada (wakazi 12,026), Pedra Badejo (wakazi 9,345) na São Filipe (wakazi 8,125).

Historia

Hadi kufika kwa Wareno katika karne ya 15 visiwa vya Cabo Verde havikuwa na watu.

Wareno walianzisha mashamba ya miwa na kuleta watumwa kutoka bara la Afrika.

Cabo Verde ilikuwa pia kituo muhimu cha biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika.

Wahamiaji kutoka Ulaya walikuwa pia Wahispania, Waitalia pamoja na Wayahudi na Waislamu waliokataliwa kukaa kwao Ureno.

Watu

Kutokana na historia hiyo, leo idadi kubwa ya wakazi ni machotara waliozaliwa na Waafrika (waliochangia 56% ya DNA) na Wazungu (waliochangia 44%).

Lugha rasmi ni Kireno, lakini wakazi wanazungumza zaidi aina mbalimbali za Krioli iliyotokana na lugha hiyo.

Upande wa dini, walau 89.1% ya wakazi ni Wakristo, hasa wa Kanisa Katoliki (78.7%), lakini pia wa madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (10.4%).

Kutokana na hali ngumu ya uchumi, wananchi wanaoishi nje ya Cabo Verde ni mara mbili kuliko wale wanaoishi nchini. Kati ya waliohama baada ya uhuru (1975), 500,000 wanaishi Marekani na 150,000 Ureno. Hata hivyo kuna wahamiaji vilevile, hasa kutoka nchi za Afrika bara.

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Cabo Verde kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.