Kiashiria cha Maendeleo ya Watu

Kiashiria cha Maendeleo ya Watu (Kiingereza: Human Development Index; kifupi: HDI) ni namba ya takwimu ambayo inaashiria ubora wa elimu, matarajio ya muda wa kuishi, na pato kwa kila mtu na hutumika ili kuweka nchi katika safu nne za maendeleo. Nchi hufanikisha kiashiria bora ikiwa na elimu bora, muda mrefu wa kuishi, na pato kubwa la wastani.

World map
Ramani ya nchi kulingana na maendeleo (kutokana na data za 2022, ilichapishwa mnamo 2024).
  •      ≥ 0.950
  •      0.900–0.950
  •      0.850–0.899
  •      0.800–0.849
  •      0.750–0.799
  •      0.700–0.749
  •      0.650–0.699
  •      0.600–0.649
  •      0.550–0.599
  •      0.500–0.549
  •      0.450–0.499
  •      0.400–0.449
  •      ≤ 0.399
  •      Hakuna data

Kiliendelezwa na mchumi Mpakistani Mahbub ul-Haq kikatumiwa sana na Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ili kupima maendeleo.

Safu za maendeleo ni duni (<0.550), wastani (0.550-0.699), juu (0.700-0.799), na juu sana (>0.800).[1]

Marejeo

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiashiria cha Maendeleo ya Watu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.