Maangamizi ya Waarmenia
Maangamizi ya Waarmenia (kwa Kiarmenia Հայոց Ցեղասպանություն, Hayots Tseghaspanutyun) maarufu kwa Kiingereza kama Armenian Holocaust,[1], Armenian Massacres na kwa Kiarmenia Մեծ Եղեռն, Medz Yeghern, "Ovu kubwa")[2],[3] yalikuwa sera ya Dola la Osmani ya kukomesha Waarmenia wote walioishi ndani ya eneo la dola hilo (leo nchini Uturuki.
Makadirio ya waliouawa ni kati ya watu milioni 1 na 1.5.
Tarehe inayohesabiwa kuwa mwanzo wa hayo mauaji ya kimbari ni 24 Aprili 1915, ambapo watawala Waturuki waliteka wasomi Waarmenian 250 mjini Istanbul. Tarehe hiyohiyo miaka 100 baadaye yalifanyika maadhimisho makubwa katika nchi mbalimbalimbali, hasa huko Etchmiadzin, makao makuu ya kiroho ya Waarmenia, ambapo Patriarki Katolikosi Karekin II aliwatangaza kwa jumla waliouawa kuwa watakatifu wafiadini.
Maangamizi yalitekelezwa kwa awamu mbili: kwanza wanaume wazima waliuawa mara moja au kulazimishwa kufanya kazi za shokoa, halafu wanawake, watoto, wazee na wagonjwa waliswagwa na wanajeshi hadi jangwa la Syria ili wafe njiani, baada ya kunyimwa chakula, maji, mbali ya kuibiwa, kubakwa na kuuawa.[4][5][6]
Makabila mengine pia, hasa ya Kikristo, kama vile Waashuru na Wagiriki, waliangamizwa na Waturuki wakati huohuo.
Mtawanyiko wa Waarmenia duniani unatokana kwa kiasi kikubwa na mauaji hayo.
Vilevile ni kutokana nayo kwamba Raphael Lemkin alitunga neno genocide mwaka 1943 kama maangamizi ya halaiki ya mpango na kadiri ya sera.[7]
Maangamizi hayo yanahesabiwa ya kwanza katika karne ya 20[8][9][10] yakifuatwa na yale makubwa zaidi ya maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya chini ya Adolf Hitler.[11]
Uturuki, ulioshika nafasi ya Dola la Osmani, unazidi kukataa neno genocide kuhusiana na mauaji ya Waarmenia, ingawa wataalamu wengi wa historia wanaliona kuwa sahihi na nchi nyingi zaidi na zaidi zinaudai ukiri kosa na kupatana na Waarmenia.[12]
Picha
- Waarmenia wakikimbia trenini
- Waarmenia waliokatwa vichwa
- Watoto wakimbizi huko Aleppo
- Mwarmenia mwanamke akiteswa karibu na mtoto aliyeuawa
- Askari wakicheza na mafuvu ya vichwa vya Waarmenia
- Umati wa Waarmenia walioagizwa kukusanyika halafu wakaangamizwa
- Mwanamke Mwarmenia akiwalilia watoto wake watano waliouawa
- Uhamisho wa Waarmenia. Askari amewaibia.
- Kambi la wakimbizi huko Syria
- Maiti za watoto Waarmenia
- Wakimbizi Waarmenia huko Hauran, Syria, wakila mzoga wa farasi
- Maiti huko Diyarbakir
- Waarmenia wakinyongwa na Waturuki
- Uhamisho wa Waarmenia katika wilaya ya Mamuret Al-Aziz
- Uhamisho wa Waarmenia
- Near East Relief na wakimbizi Waarmenia huko Bitlis
- Mwanamke Mwarmenia na mwanae
- Waarmenia waliokimbilia hospitali ya American Relief eye
- Wakimbizi kwenye Near East relief
- Ugawaji wa chakula
- Mwanamke na mtoto
- Kwenda Ugiriki
- Watoto kwenye Near East Relief
- Kwenda Ugiriki
- Waarmenia waliokamatwa kabla hawajaangamizwa
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
- The Armenian Genocide Institute-Museum, Yerevan, AM.
- Armenian National Institute, Washington, D.C. (dedicated to the study, research, and affirmation of the Armenian Genocide).
- Armenian Genocide Debate.
- The Forgotten, videos of interviews with survivors.
- "Armenians 1915", Armenian Genocide Research Center (World Wide Web log), Google Bogger.
- "Fall of the Ottoman Empire", Online Encyclopedia of Mass violence (chronological index & articles).
- Genocide, AM, ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-12-05, iliwekwa mnamo 2015-04-18.
- "Screamers", You tube (video) (documentary), Google, about genocide, featuring System of a Down.
- .
- Pope John Paul II and Pope Francis on the Armenian Genocide
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Maangamizi ya Waarmenia kama enzi zake au matokeo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |