Papa Leo IV

Papa Leo IV, O.S.B. alikuwa Papa kuanzia mwezi Januari au tarehe 10 Mei 847 hadi kifo chake tarehe 17 Julai 855[1]. Alitokea Roma, Lazio, Italia[2].

Mt. Leo IV.

Alimfuata Papa Sergio II akafuatwa na Papa Benedikto III.

Kutokana na uvamizi na uharibifu wa Roma uliofanywa na Waarabu, aliimarisha boma la mji na kulipanua hadi kandokando ya Vatikano[3][4], alikarabati makanisa kadhaa, yakiwemo Basilika la Mt. Petro na Basilika la Mt. Paulo, halafu alihamasisha falme za Kikristo kupambana nao[5].

Mwaka 849, meli za Kiislamu zilipokaribia pwani ya Italia ya Kati, alihamasisha jamhuri za kibahari za Napoli, Gaeta na Amalfi kuungana dhidi ya hatari hiyo mpya. Mapigano ya Ostia yalileta ushindi mkubwa[6][7].

Pamoja na kulinda mji wa Roma, alitetea mamlaka ya Papa kwa mwandamizi wa Mtume Petro[8]

Kanisa Katoliki linamheshimu kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 17 Julai[9].

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Marejeo

  • Cheetham, Nicolas, Keepers of the Keys, New York: Charles Scribner's Sons, 1983. ISBN 0-684-17863-X

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Leo IV kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.