Sigimundi Gorazdowski

Sigimundi Gorazdowski (kwa Kipolandi: Zygmunt; Sanok, Podkarpackie, Austria-Hungaria, leo nchini Polandi, 1 Novemba 1845Lwów, leo nchini Ukraina, 1 Januari 1920) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki, mwanzilishi wa shirika la Masista wa Mt. Yosefu.[1][2]

Picha halisi ya Mt. Sigimundi.

Utotoni Gorazdowski aliugua TB hivi ilimbidi asubiri apone kabisa kabla hajapewa upadirisho.[2]

Baadaye alifanya kazi katika parokia mbalimbali akianzisha kwa huruma kubwa nyumba kwa mayatima, wasichana wenye watoto na wahitaji wengineo. Pia aliandika katekisimu na vitabu vingine vya dini kwa watu wake na kutetea uhai wa wasio na sauti.[3][4][5]

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri huko Ukraine tarehe 26 Juni 2001. Papa Benedikto XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 23 Oktoba 2005 huko Vatikano.[4]

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[6].

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.