Klorini


Klorini ni elementi yenye namba atomia 17 katika mfumo radidia maana yake kiini atomia chake kina protoni 17. Uzani atomia ni 35.453 na alama yake Cl. Ni elementi ya pili katika safu ya halojeni.

Klorini
Jina la ElementiKlorini
AlamaCl
Namba atomia17
Mfululizo safuHalojeni
Uzani atomia 35.453
Valensi1, 3, 5, 7
Ugumu (Mohs){{{ugumu}}}
Kiwango cha kuyeyuka171.6 K (−101.5 °C)
Kiwango cha kuchemka239.11 K (−34.04 °C)
Asilimia za ganda la dunia0.19 %
Hali maada gesi

Katika hali sanifu ni gesi yenye rangi njanokijani. Inamenyuka haraka na elementi nyingine na ni sumu kwa wanyama na binadamu.

Inapatikana kwa wingi katika maji ya bahari kama sehemu ya chumvi ya kawaida NaCl na pia ndani ya chumvi ya KCl.

Matumizi yake ni kusafisha maji au kung'arisha karatasi kiwandani. Imewahi kutumiwa kama sehemu ya silaha kama gesi ya sumu.

Klorini inapotumika kusafisha maji, kuna uwezekano kwamba kiasi cha klorini hubaki mwenye maji. Hivyo basi kuna mbinu mwafaka ambazo hutumika ili kusafisha hayo maji na kuondoa harufu na pia elementi za klorini. Mfano wa baadhi ya hizi mbinu ni uvukizi, klorini dioxide, kubadili myonzo, na njia ya kuchuja.

Picha

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Klorini kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.