Siku ya Ukimwi Duniani

Siku ya UKIMWI duniani huadhimishwa tarehe 1 Desemba kila mwaka ili kueneza ufahamu wa ugonjwa wa UKIMWI unaosababishwa na uambukizi wa virusi vya UKIMWI. Ni kawaida kuwa na ukumbusho huo siku hii ili kuwajali watu ambao wamefariki kutokana na VVU / UKIMWI.

Kitambaa chekundu ni ishara ya kimataifa kwa mshikamano na watu wenye VVU na wale wanaoishi na UKIMWI.

Serikali na pia maafisa wa afya huadhimisha siku hii, mara nyingi kwa hotuba au vikao kuhusu mada ya UKIMWI. Tangu mwaka 1995, Rais wa Marekani ametoa tangazo rasmi juu ya Siku ya UKIMWI Duniani. Serikali za mataifa mengine zimefuata mtindo huu na kutoa matangazo maalum.

UKIMWI umeua zaidi ya watu milioni 25 kati ya 1981 na 2007, [1] na wastani wa watu milioni 33.3 wanaishi na VVU duniani kote kutoka 2009, pamoja na 2.6 milioni kuambukizwa kila mwaka, na 1.8 milioni kufa kwa Ukimwi AIDS.[2] kuifanya kuwa moja ya magonjwa haribifu zaidi katika historia iliyoandikwa.

Licha ya kuboresha upatikanaji wa huduma ya matibabu na madawa ya kurefusha maisha katika maeneo mengi ya dunia, UKIMWI ulisababisha vifo vya watu wanaokadiriwa milioni 2 mwaka 2007, [3] na miongoni mwao 270.000 walikuwa watoto. [4]

Historia

Siku ya Ukimwi Duniani ilibuniwa mnamo Agosti 1987 na James W. Bunn na Thomas Netter, maafisa wawili wa habari kwa umma kwa ajili ya Mpango wa Kimataifa juu ya UKIMWI katika Shirika la Afya Duniani mjini Geneva, Uswisi. [5] [6] Bunn na Netter walichukua wazo lao kwa Dokta Jonathan Mann, Mkurugenzi wa Mpango wa Kimataifa juu ya UKIMWI (ambao sasa unajulikana kama UNAIDS). Dr Mann alipenda wazo lao, akaliridhia na kukubaliana na pendekezo kuwa adhimisho la kwanza la Siku ya Ukimwi Duniani iwe tarehe 1 Desemba 1988.

Bunn alipendekeza tarehe hiyo ili kuhakikisha uangalifu wa vyombo vya habari vya Ulaya, kitu ambacho aliamini kuwa muhimu kwa mafanikio ya Siku ya Ukimwi Duniani. Aliamini hivyo kwa sababu 1988 ulikuwa mwaka wa uchaguzi huko Marekani na vyombo vya habari vingekuwa vimechoka kurekodi habari za uchaguzi na wangekuwa na hamu ya kupata habari mpya. Bunn na Netter waliona kuwa 1 Desemba ilikuwa muda wa kutosha baada ya uchaguzi na mapema kabla ya likizo ya Krismasi na hakukuwa na habari kamilifu siku hiyo kwa hivyo ingekuwa siku barabara kuadhimishia Siku ya Ukimwi Duniani.

(Bunn, aliyekuwa awali mwanahabari aliyerekodi ugonjwa huu kwa KPIX-TV katika San Francisco, pamoja na mtayarishaji Nancy Saslow, pia alibuni na alianzisha "AIDS Lifeline" - kampeni ya ujulishaji wa umma na elimu ya afya iliyokuwa ikienezwa kupitia vituo vya televisheni nchini Marekani "AIDS Lifeline "ilipewa tuzo ya Peabody, tunu la kienyeji, na Tuzo ya kwanza ya Taifa kuwahi kupewa kituo cha habari nchini Marekani

Tarehe 18 Juni 1986 "AIDS Lifeline" iliheshimiwa kwa ungamo la Rais kwa mipango katika Sekta Binafsi, ilipewa na Rais Ronald Reagan. Bunn kisha aliombwa na Dr Mann, kwa niaba ya serikali ya Marekani, kuchukua miaka miwili idhini-ya-kutokuwepo ili ajiunge na Dr Mann (daktari wa ngozi katika Centers for Disease Control) ili kusaidia katika kubuni Mpango wa Kimataifa juu ya UKIMWI. Bunn alikubali na akawa Afisa wa Habari za Umma wa kwanza wa mpango wa UKIMWI duniani. Pamoja na Netter wali buni, wakaunda, na kutekeleza maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani - sasa ni mpango wa ufahamu na kinga kuu zaidi katika historia ya afya ya umma.)

Ungano wa mpango wa Umoja wa Mataifa juu ya UKIMWI (UNAIDS) ulianzishwa mwaka 1996, na ukasimamia mipango na uendelezaji wa Siku ya Ukimwi Duniani. [7] Badala ya kuzingatia siku moja, UNAIDS iliumba Kampeni ya Ukimwi Duniani mwaka 1997 kwa lengo la kueneza mawasiliano, kuzuia na kuelimisha mwaka mzima. [7] [8]

Katika miaka miwili ya kwanza, maudhui ya Siku ya Ukimwi Duniani yalilenga watoto na vijana. Mandhari haya yalikosolewa sana wakati huo kwa sababu ya kupuuza ukweli kwamba watu wa umri wowote wanaweza kuambukizwa na VVU na kuteseka kutokana na UKIMWI. [7] Lakini mandhari yalizingatia VVU / UKIMWI, ilisaidia kupunguza unyanyapaa unaoathiri ugonjwa huo, na ilisaidia kukuza ufahamishaji kwa tatizo hilo kama ugonjwa wa familia. [7]

Mwaka 2004, Kampeni ya Ukimwi Duniani ikawa shirika la kujitegemea. [7] [8] [9]

Kila mwaka Papa Yohane Paulo II na Papa Benedikto XVI wametoa ujumbe wa kuwaamkia wagonjwa na madaktari Siku ya Ukimwi Duniani. [10] [11] [12][13]

Kuchagua maudhui

Tangu ianzishwe mpaka 2004, UNAIDS imeongoza kampeni ya Siku ya Ukimwi Duniani, ikichagua maudhui ya mwaka kwa kushauriana na mashirika mengine ya afya ya kimataifa.

Kufikia 2008, kila mwaka maudhui ya Siku ya Ukimwi Duniani huchaguliwa na kamati ya Kampeni ya Ukimwi duniani baada ya kushauriana na watu, mashirika na mawakala wa serikali wanaohusika katika kuzuia ugonjwa na kutoa matibabu ya VVU / UKIMWI. [7] Kwa kila Siku ya Ukimwi Duniani kuanzia mwaka 2005 kupitia 2010, maudhui itakuwa "Zuia Ukimwi. Timiza Ahadi." [7] Maudhui haya makuu yameundwa ili kuhamasisha viongozi wa kisiasa kuweka ahadi zao ili kufanikisha upatikanaji wa matibabu, huduma na msaada dhidi ya VVU / UKIMWI, kabla ya mwaka 2010. [7]

Maudhui haya si mahususi kwa Siku ya Ukimwi Duniani, lakini hutumika mwaka mzima katika jitihada za WAC kusisitiza ufahamu wa VVU / UKIMWI ndani ya mazingira ya matukio mengine makubwa duniani ikiwemo mkutano wa G8. Kampeni ya UKIMWI duniani pia inafanya kampeni za "ndani ya nchi" duniani kote, kama Student Stop AIDS Campaign, kampeni ya kufamisha watu juu ya uambukizaji na uepukaji, linalolenga vijana kote Uingereza.

Kitambaa kikubwa chekundu kinaning'inia kati ya nguzo katika kaskazini ya portico ya White House kwa ajili ya Siku ya Ukimwi Duniani, 30 Novemba 2007
"Mpira" wa urefu wa mita 67 Uwanja wa Buenos Aires, Argentina, mojawapo ya kampeni ya 2005 kwa Siku ya Ukimwi Duniani
Maudhui ya Siku ya Ukimwi Duniani 1988 - sasa [14]
1988Mawasiliano
1989Vijana
1990Wanawake na Ukimwi
1991Kushirikiana katika Tatizo
mwaka wa (1992).Jamii Kuungama
1993Tenda
1994UKIMWI na Familia
1995Mgawanyo wa Haki, Mgawanyo la Jukumu
mwaka wa (1996).Dunia Moja. Tumaini Moja
1997Watoto Kuishi katika Dunia na UKIMWI
1998Shinikiza mageuzi: Kampeni ya Ukimwi Duniani na vijana
1999Kusikiliza, Kujifunza, Kuishi: Kampeni ya UKIMWI duniani na watoto na vijana
2000UKIMWI: Wanaume Tufanye Mabadiliko
2001Najali. Je wewe?
2002Unyanyapaa na ubaguzi
2003Unyanyapaa na ubaguzi
2004Wanawake, wasichana, VVU na UKIMWI
2005Komesha UKIMWI. Timiza Ahadi
2006Komesha UKIMWI. Timiza Ahadi - Uwajibikaji
2007Komesha UKIMWI. Timiza Ahadi - Uongozi
2008Komesha UKIMWI. Timiza Ahadi - Ongoza - Ezesha - Tekeleza [15]
2009Upatikanaji duniani na Haki za Binadamu [16]

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje